HOME

Jan 20, 2012

WATU 6 WAUWA MJINI MOGADISHU!!


Mlipuko wa Bomu umetokea ndani ya kambi iliyofurika katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu, muda mfupi baada ya kundi la maafisa wa Umoja wa Mataifa kuondoka mahali hapo.


Takriban watu sita wamefariki na inahofiwa idadi hiyo ikaongezeka kwani watu wengi zaidi wamejeruhiwa.


Mlipuko huo ulitokea muda mfupi baada ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa na waandishi wa Habari wa kimataifa kuzuru eneo hilo.

No comments:

Post a Comment