HOME

Jan 27, 2012

WAGONJWA WAKOSA HUDUMA KUFUATIA MGOMO WA MADAKTARI MOROGORO!!

Mgomo wa madaktari katika hospitali ya mkoa wa Morogoro umeendelea ambapo baadhi ya wagonjwa waliolazwa katika hospitali wakilalamika kukosa huduma za matibabu huku wakishuhudia vifo kutokea kwa kukosa huduma

Mwandishi wa habari hizi ameshuhudia vyumba vya madaktari vikiwa tupu na huduma za matibabu kutotolewa na kusababisha hali kuwa mbaya zaidi kwa wagonjwa waliolazwa wodini wakiwemo watoto wadogo ambao hawajahudumiwa tangu jana huku baadhi wakikiri kushuhudia  vifo  vya wagonjwa kwa kukosa huduma na baadhi wakitaka waruhusiwe kwenda hospitali binafsi kupata matibabu.

Kwa upande wa wagonjwa wa nje waliokuwa kwenye foleni kutoka wilayani ambao matibabu yao yalishindikana huko wilayani na kulazimika kuhamishishwa katika hospitali ya  mkoa wa Morogoro wamelalamikia kukosa huduma kutwa nzima na hawajui hatma ya matibabu yao.

No comments:

Post a Comment