Petra Kvitova |
Bingwa wa Wimbledon Petra Kvitova amenusurika na hatimae kufanikiwa kutinga nusu fainali ya shindano la wazi la Australia baada ya kumfunga Sara Errani .
Sara ambaye hayupo katika ubora kiviwango katika michuano hiyo aliongoza kwa 4-1 seti ya kwanza na kumweka katika hali ngumu Kvitova ambaye aliweza kujikwamua na kumaliza seti hiyo kwa 6-4.
Katika seti ya pili bado Kvitova alikumbana na ushindani mkubwa na kumaliza mchezo wa seti 6-4 6-4 na anatarajiwa kupambana na Maria Sharapova mchezo wa nusu fainali.
No comments:
Post a Comment