HOME

Jun 30, 2012

SHUHUDIA INAVYOKUWA KWENYE DANCE 100% YA EATV!!

Dj Summer kutoka EA RADIO na EATV


Mchakato wa kusaka makundi bora ya ku-dance jijini Dar es Salaam unaofahamika kama Dance 100% umeweza kuvutia umati mkubwa uliojitokeza kushiriki na kushuhudia michuano mikali ambayo imefanikisha kupatikana na makundi 17 yaliyoonekana kufikia kiwango kilichorodhisha waamuzi.

Mpango mzima wa Dance Miamia ulianza kwa kasi kubwa ndani ya viwanja vya Leaders Club Kinondoni, na kufuatiwa na uwanja wa Don Bosco Wilayani Ilala na kuishia Wilaya ya Temeke ndani ya uwanja wa TCC Changombe.
Majaji wa mashindano hayo ni wakali wenye experience Lotus Kyamba kutoka EATV ambaye alianza kudance tangu akiwa na umri wa miaka mitano,Super Nyamwela wa Extra Bongo mwenye Experience ya kutosha pamoja na mkali Prince Dully Sykes.

Utaratibu wa kutoa marks ulikuwa kama hivyo kwa kutumia vibao vyenye asilimia 10 mpaka 100 kama shindano linavyosema.



Usikose kuangalia show hii kali ya Dance Mia Mia kila Jumatano saa 3 na nusu usiku ili ujionee mwenyewe kilivyosanuka kuanzia pale viwanja vya Leaders Club Kinondoni,Ilala na baadae Don Bosco Jijini Dar es Salaam, kupitia EATV Pekee!!!

No comments:

Post a Comment