HOME

May 29, 2013

PICHA: HUZUNI KWA WASANII, CHEMBA SQUARD WAKIWA STUDIO EAST AFRICA RADIO!!

Wasanii wa karibu sana wa msanii Albert Mangwea waliofahamika kama Chemba Squad leo walipata nafasi ya kufika katika studio za East Africa Radio kumzungumzia kwa kifupi Marehemu ambapo walionekana kuwa na huzuni kubwa sana kumpoteza mwana kundi mwenzao.
Kushoto Dogo Hamidu ambaye alikuja kuzungumzia maisha ya wabongo nchini Afrika Kusini ambapo amezungumza mengi na kulia ni Mchizi Mox ambaye amekuwa busy kushughulikia taratibu nzima za msiba wa rafiki yake Ngwair ambapo amehamasisha wadau kukutana leo saa 10 jioni pande za Leaders Club ili kuzungumza kuhusu msiba huo
Noorah pamoja na Mez B wakiwa ndani ya studio
Mchizi Mox
Mez B akiwa katika majonzi ambaye hapo alipo anaumwa lakini amejitahidi ili kuja kutoa salamu zake za pole kwa ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu Albert Mangwea.
Watangazaji wa kipindi cha Power Jams Sam Misago na Ana Peter wakiwa kwenye show
Mchizi Mox akimzungumzia marehemu na historia yao kwa ufupi jinsi walivyokutana na marehemu pamoja na taratibu za msiba kwa ufupi.

DJ Kim

No comments:

Post a Comment