HOME

Jan 27, 2012

TUCTA YAINGILIA KATI MGOMO WA MADAKTARI!!

Katibu mkuu wa TUCTA, Bw. Nicolas Mgaya,

Shirikisho la vyama vya wafanyakazi nchini Tanzania (TUCTA) limeunga mkono mgomo wa nchi nzima unaofanywa na madaktari na wanataaluma wa afya na kuitaka serikali kushughulikia madai ya madaktari hao sambamba na kushughulikia madai ya wafanyakazi kutoka kada nyingine katika jamii.


Katibu mkuu wa TUCTA, Bw. Nicolas Mgaya, amesema kuwa madai ya wanataaluma wa afya ni sehemu tu ya madai ya muda mrefu yanayotolewa na wafanyakazi nchini na kwamba kuna haja ya serikali kutopuuzia madai hayo.


Wakati Bw. Mgaya akitoa msimamo wa TUCTA, upatikanaji wa huduma za afya katika zahanati na hospitali za umma sehemu mbali mbali nchini, umezidi kuzorota, hasa baada ya kuwepo kwa taarifa kuwa madaktari katika hospitali ya mkoa wa Morogoro nao wamejiunga na mgomo huo.

No comments:

Post a Comment