HOME

Jan 26, 2012

RAIS KIBAKI AMFUKUZA KAZI NAIBU JAJI MKUU!!

Naibu Jaji Mkuu aliyefukuzwa kazi Nancy Baraza

Rais Mwai Kibaki wa Kenya jana amemsimamisha kazi Naibu Jaji Mkuu Nancy Baraza na kuunda jopo ambalo litafanyia uchunguzi mwenendo wake kutokana na shutuma zinazomkabili.


Jopo hilo litaongozwa na aliyekuwa Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Augustino Stephen Lawrence  Ramadhan kama Mwenyekiti.


Jaji Baraza, anashutumiwa kumtishia maisha kwa bastola mlinzi wa duka moja kubwa, Bi Rebecca Kerubo wakati wa mkesha wa mwaka mpya.

No comments:

Post a Comment