HOME

Feb 1, 2012

POLISI KENYA INAMSAKA MTOTO WA RUPIAH BANDA!!

Henry Banda

Jeshi la polisi nchini Kenya limejiunga katika msako wa mtoto wa rais wa zamani wa Zambia Rupiah Banda ambaye anadaiwa kuwepo nchini Kenya.


Jeshi la polisi nchini Zambia limetoa hati ya kimataifa ya kukamatwa kwa Henry Banda kufuatia ripoti kuwa amesafiri kutoka Afrika kusini kwenda Kenya baada ya kugundua kuwa anatafutwa kufuatia uchunguzi unaoendelea wa fedha za baba yake za kampeni.


Inspekta generali wa polisi wa Zambia Martin Malama amebainisha kuwa Henry yupo nchini Kenya na kumuonya ajisalimishe kuliko kuendelea kucheza mchezo wa kujificha na sheria.

No comments:

Post a Comment