HOME

Feb 17, 2012

RAIA WA NIGERIA WA KUNDI LA AL-QAEADA AFUNGWA MAISHA!!




















Raia mmoja wa Nigeria anayetuhumiwa kujaribu kulipua ndege inayokwenda Marekani siku ya Krismasi mwaka 2009, amehukumiwa kifungo cha kwenda jela maisha.


Umar Farouk Abdulmutallab, 25, alikiri kosa la kujaribu kulipua ndege ya abiria akiwa kama mfuasi wa kundi na kutekeleza njama za al-Qaeda.


Familia yake mara moja imetaka serikali ya Marekani kupitia upya hukumu hiyo.


Abdulmutallab aliungua wakati bomu lililokuwa limeshonwa ndani ya nguo yake ya dani kushindwa kulipuka kikamilifu, wamesema waendesha mashtaka.


Watu wapatao 300 walikuwemo ndani ya ndege hiyo ikitokea Amsterdam kwenda Detroit.


Baadhi ya abiriwa walikuwepo mahakamani hapo wakati jaji Nancy Edmunds akitoa hukumu hiyo.

No comments:

Post a Comment