HOME

Feb 1, 2012

ICTR YAWAOMBEA HIFADHI WALIOACHIWA HURU!!


Mahakama inayoendesha kesi za mauaji ya kimbari yaliyotokea Rwanda mwaka 1994 imetoa wito kwa mataifa kutoa hifadhi kwa wale walioondolewa mashtaka.


Watu 5 kati ya watu 10 walioondolewa lawama za kuhusishwa katika mauaji hayo wanasema hawawezi kurejea nchini Rwanda.


Wanaishi chini ya ulinzi wa Polisi katika nyumba moja mjini Arusha, Tanzania, ambako ndiko makao ya mahakama hiyo ya ICTR.


Mahakama hiyo ya ICTR inatarajiwa kufunga mwishoni mwa mwaka huu.

No comments:

Post a Comment