HOME

Feb 6, 2012

COMING SOON:”RESPECT NYERERE” FROM STEVE NYERERE!!



Siku chache zijazo,msanii Steve Nyerere,ambaye yaelekea ameamua kujikita katika filamu zenye uhalisia fulani hususani zenye mrengo wa kisiasa,anatarajiwa kuzindua filamu yake mpya inayokwenda kwa jina Respect Nyerere ikiwa ni filamu kuhusu baadhi ya matukio au mambo yatokanayo na maisha ya Baba wa Taifa,Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.


Steve Nyerere ambaye hivi karibuni alitoa filamu ya Mr.President ambayo ni filamu yenye matukio sambamba na maisha ya Rais wa sasa,Jakaya Mrisho Kikwete,amesema filamu ya Respect Nyerere itazinduliwa rasmi tarehe 14 Februari 2012 katika Hotel ya Serena jijini Dar-es-salaam.

No comments:

Post a Comment