HOME

Feb 3, 2012

MABOMU YA MACHOZI YATAWALA MISRI!!



Waandamanaji waliokasirishwa na vifo vya watu 74 baada ya mchezo wa kandanda katika mji wa Port Said nchini Misri siku ya Jumatano wamepambana na polisi nje ya wizara ya mambo ya ndani mjini Cairo.


Kituo cha TV cha serikali kimesema mamia ya watu wamejeruhiwa katika tukio hilo.


Mapema, waziri mkuu wa Misri alitangaza kuwafukuza kazi maafisa wa ngazi za juu mjini Port Said na pia katika chama cha soka cha Misri.

Mazishi ya baadhi ya waliokufa yamefanyika katika mji wa Port Said.

No comments:

Post a Comment