HOME

Feb 9, 2012

IVORY COAST KUKUTANA NA ZAMBIA FAINALI!!


Ivory Coast itakutana na Zambia kwenye fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya timu hizo mbili kushinda mechi zao za nusu fainali.


Ivory Coast imefuzu baada ya kuishinda Mali 1-0 katika nusu fainali yao mjini Libreville, nchini Gabon.


Bao la ushindi la Ivory Coast lilifungwa na mchezaji wa Arsenal Gervinho katika kipindi cha pili.


Awali katika mji wa Bata nchini Gabon Zambia iliibandua Ghana kutoka mashindano hayo kwa kuifunga 1-0.


Bao la Zambia lilifungwa katika dakika ya 78 na mshambuliaji Emmanuel Mayuka.

No comments:

Post a Comment