HOME

Feb 16, 2012

MAMIA YA WAFUNGWA WATEKETEA HONDURAS!!


Takriban wafungwa 300 wameuwawa katika moto ulioteketeza jela moja nchini Honduras kwa mujibu wa maafisa wa serikali.


Wengi wao waliteketea au kukosa hewa katika seli zao za jela ya Comayagua, kaskazini mwa mji mkuu Tegucigalpa.


Maafisa wa serikali wanasema imethibitishwa takriban 300 wamekufa lakini wengine 56 kati ya wafungwa 853 katika gereza hilo hawajapatikana na inadhaniwa wameteketezwa.


Jamaa wa wafungwa hao walipambana na polisi pale walipojaribu kuvamia jela hiyo wakitafuta maelezo zaidi ya majaaliwa ya watu wao.

No comments:

Post a Comment