HOME

Feb 1, 2012

CHADEMA YAITAKA SERIKALI KUREJEA KWENYE MAZUNGUMZO NA MADAKTARI!!

Mkurugenzi wa habari na uenezi chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Bw  John Mnyika

Chama cha  demokrasia na maendeleo Tanzania (CHADEMA)  kimeitaka serikali  kurudi kwenye meza ya mazungumzo  na madaktari na kutumia  rasilimali zilizopo  kutatua madai ya madaktari nchini

Hayo yameelezwa Mkoani morogoro katika kongamano la katiba mpya kwa wananfunzi wa vyuo chuo kikuu Mzumbe ambapo  mkurugenzi wa habari na uenezi chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Bw  John Mnyika amesema kukosekana kwa uadilifu rasilimali zilizopo nchini zinashindwa kuwanufanisha watanzania

Nae Mkurugenzi wa sheria na haki za binadamu  CHADEMA Tundu Lissu akizungumzia kuhusu
katiba mpya amesema watanzania wanahitaji katiba mpya yenye  mabadiliko ya kubadilisha nchi  na kuongeza uwajibikaji wa viongozi kwa wananchi.

No comments:

Post a Comment