Feb 3, 2012
WAVUVI WATAKIWA KUACHA KUTUMIA ZANA HARAMU.
Wavuvi nchini Tanzania wametakiwa kuacha kutumia zana haramu za uvuvi kwasababu zinasababisha kuvua samaki wadogo na kuangamiza wengine ambao wangeweza kukuwa na kuongeza pato la nchi.
Hayo yamesemwa na Meya wa manispaa ya Singida Alhaji Salumu Mahami wakati alipokuwa akichoma moto makokolo na neti ya mbu zenye matundu madogo zilizokuwa zikitumiwa na wavuvi wa bwawa la Singida kuvulia samaki kinyume na sheria.
Mahami amesema kitendo cha kuvua samaki wakiwa bado wadogo kinalikosesha taifa fedha nyingi, kwahiyo amewaomba wananchi na wavuvi kushirikiana na wataalamu wa uvuvi iliwaweze kufuata sheria za uvuvi kwa ajili ya manufaa ya taifa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment