HOME

Apr 26, 2012

WAWILI WAFARIKI DUNIA KATIKA MATUKIO MAWILI TOFAUTI MKOANI SONGEA!!

Kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda
Watu wawili wamefariki dunia katika matukio tofauti wilayani Songea mkoani Ruvuma likiwemo la mtoto mwenye umri wa miaka miwili kufariki baada ya kutumbukia kwenye kisima cha maji huku mmoja mwenye umri wa miaka themanini akifariki dunia baada ya kugongwa na gari ambalo halikuweza kufahamika mara moja.


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda ni kuwa tukio la kwanza la mtembea kwa miguu Kanisia Nyoni(80) kugongwa na gari na kufariki dunia papo hapo lilitokea katika eneo la kata ya Tanga nje kidogo ya mji wa Songea.


Amesema kuwa mtu huyo alipatwa na ajali hiyo katika bara bara ya Songea-Makanbako ambapo gari lililokuwa katika mwendo kasi majira ya saa moja usiku lilimgonga Bi. kizee huyo aliyekuwa akirejea nyumbani kwake na jeshi la polisi mkoani Ruvuma linaendelea kufanya uchunguzi ili kulibaini gari hilo lililohusika katika ajali hiyo.

No comments:

Post a Comment