HOME

Apr 13, 2012

JARIBIO LA KURUSHA ROKETI KOREA KASKAZINI LIMEFELI!!

Jaribio la Korea Kaskazini kurusha roketi, ambalo limekuwa likifuatiliwa kwa ukaribu na mataifa mbalimbali, limefeli.


Jaribio hilo linalochukuliwa na Marekani na baadhi ya mataifa ya Asia kama jaribio la kurusha kombora la masafa marefu, lilifanyika kaskazini magharibi mwa nchi hiyo mapema leo asubuhi.


Marekani, Japan na Korea KUsini zimesema roketi hilo liliruka kwa muda mfupi kabla ya kulipuka na kuanguka baharini katika peninsula ya Korea.

No comments:

Post a Comment