HOME

Apr 13, 2012

WANASIASA NCHINI KENYA WATAKIWA KUACHA KAMPENI ZA KISIASA KATIKA MASUALA YA NCHI!!

Rais Mwai Kibaki wa Kenya
Rais Mwai Kibaki wa Kenya amewataka viongozi wa ngazi zote nchini humo kujiepusha na kampeni za kiasiasa zinazorudisha nyuma uchumi wa nchi na agenda nzima ya maendeleo kwa ujumla.


Rais Kibaki amewaomba viongozi kuepuka malumbano yasiyo ya lazima ambayo yanaiweka nchi hiyo katika presha ya uchaguzi mkuu na badala yake watilie mkazo masuala mazuri yenye manufaa kwa wananchi na nchi kwa ujuma.


Akizungumza wakati wa hafla ya chakula cha mchana iliyoandaliwa rasmi kwa heshima ya Kamishna mkuu wa mamlaka ya mapato nchini Kenya (KRA) Bw. Michael Waweru na maafisa wengine wa ngazi ya juu waliostaafu iliyofanyika katika hoteli ya   Crowne rais Kibaki amewataka viongozi kuelekeza nguvu zao katika masuala yanayoihusu jamii na hatma ya baadae ya nchi hiyo na kuepuka mambo yanayoharibu maisha ya wananchi.

No comments:

Post a Comment