HOME

Apr 26, 2012

RAIS WA MPITO MALI ATANGAZA BARAZA LA MAWAZIRI!!

Rais wa mpito Diouncounda Traore,
Rais wa serikali ya mpito wa Mali ametangaza serikali mpya,kwa kuwapa madaraka wanajeshi.


Wawakilishi wa majeshi wamepewa nyadhifa za Wizara ya Ulinzi, Wizara ya usalama wa nchini na masuala ya nchini.


Askari waliipindua serikali iliyochaguliwa kwa njia ya kidemokrasi takriban mwezi mmoja uliopita.


Viongozi wa mapinduzi hayo baadaye waliamua kukabidhi madaraka kwa Rais wa mpito Diouncounda Traore, aliyewajibishwa kuona kua ratiba ya uchaguzi inapangwa na kutekelezwa.


Mpango huu ulifikiwa na Shirikisho la kimkoa la Ecowas ambalo lilitaka kuhakikisha kwamba madaraka yarejeshwe kwa serikali itakayochaguliwa kwa kura.

No comments:

Post a Comment