HOME

Apr 24, 2012

HUDSON ATOA USHAHIDI MAHAKAMANI!!

Jennifer Hudson
Mwanamuziki Jennifer Hudson amepata wakati mgumu mahakamani hasa baada ya kushindwa kujizuia na kumwaga chozi  wakati alipokuwa akitoa ushahidi wake katika kesi inayoendelea ikimkabili aliyekuwa mume wa dada yake William Balfour kwa kuhusika na kuwaua wanafamilia yake watatu.


Hudson aliangia kilio hicho baada ya mwendesha mashtaka kumuuliza ni lini mara ya mwisho kuonana na ndugu zake hao na hasa pale alipoonyeshwa picha ya mama yake wakati akitoa maelezo ya ushahidi wake  jambo ambalo limegusa hisia za wengi.


Hudson katika ushahidi wake aliweka wazi kuwa, tangua awali hakuna hata mmoja wa wanafamilia yake aliyekuwa ameridhia swala la dada yake kujiingiza katika mahusiano na mtuhumiwa huyo wa mauaji William Balfour kutokana na kumuona kuwa ni mtu aliyekuwa na tabia za ajabu.

No comments:

Post a Comment