HOME

Apr 11, 2012

MOTO ULIVYOTEKETEZA MADUKA ,HOTEL NA BAA ARUSHA!!

Moto ulioibuka katika nyumba moja iliyoko mtaa wa Majengo katikati ya jiji la Arusha umeteketeza  maduka nane,hoteli  na baa na kusababisha hasara ya mamilioni ya fedha.

Moto huo ambao chanzo chake halisi hakijajulikana  unaodaiwa kuanzia kwenye moja ya maduka yaliyoko kwenye nyumba hiyo pamoja na kubainika mapema  ulisambaa kwa kasi kubwa licha yakuwepo kwa jitihada za kuudhibiti kutoka kwa wananchi  na kikosi cha zima moto cha Manispaa ya Arusha.

Hata hivyo jithada hizo hazikuweza kuzaa matunda kutokana na changamoto mbali mbali ikiwemo ya vitendea kazi na gari la zima moto kuishiwa  maji hadi vikosi  vingine vilipofika ika eneo hilo kutoa msaada kikiwemo kikosi cha Halmashauri  ya Wilaya ya Arumeru  na kikosi binafsi cha Night Support  cha jijini Arusha.

No comments:

Post a Comment