HOME

Apr 26, 2012

ROMA KUTENGENEZA DOCUMENTARY YA MAISHA YAKE!!

Roma (kati) akiwa na Ma presener wakali kutoka EATV Lotus Kyamba (kushoto) wa kipindi cha Nirvana kila Jumanne saa moja usiku na Baby Drama Faiza wa 5Selekt kila siku za wiki Jumatatu mpaka Ijumaa saa @1500 -1700hrs.
Msanii anayeng'ara katika anga za muziki nchini Tanzania na kuwakilisha mkoa wa  Tanga Roma mkatoliki ameweka bayana kuwa,baada ya kuchukua tuzo mbili za muziki za Kilimanjaro Music Awards hivi karibuni kama Msanii bora wa Hip Hop na wimbo wake Mathematics kuchukua kama wimbo bora wa Hip Hop hivi sasa anatengeneza Documentary yake inayoeleza maisha yake kimuziki toka alivyoanza mziki shida alizopitia mpaka kufikia hivi sasa alipofikia. 

Roma ambae pia utamshuhudia katika Kili Tour inayoanza Jumamosi mkoani Dodoma na kuzunguka katika mikoa kadhaa akiwa pamoja na wakali wengine wa muziki Tanzania walioshinda tuzo hizo amefunguka kuwa ni mapema sana kusema itatoka lini ila haitochelewa kutokana kuwa anaamini watu wataipenda na italeta utofauti kidogo maana story iliyomo ndani ya Documentary hiyo iko kitofauti na itamgusa kila mmoja.

No comments:

Post a Comment