HOME

Apr 29, 2013

WATUMISHI WAZEMBE WALA RUSHWA KUADHIBIWA!!

Watumishi wa umma nchini Tanzania wametakiwa kuacha vitendo vya rushwa na kufanya kazi kwa mazoea ili kuiwezesha nchi kufikia malengo ya maendeleo ya muda mrefu.
Waziri wa nchi ofisi ya rais Utumishi Celina Kombani akifungua mafunzo kwa maofisa waandamizi wa umma kuhusu namna wanavyoweza kutekeleza majukumu yao leo jijini Dar es salaam.
Waziri wa nchi ofisi ya rais Utumishi Celina Kombani akifungua mafunzo kwa maofisa waandamizi wa umma kuhusu namna wanavyoweza kutekeleza majukumu yao.
Baadhi ya maofisa waandamizi wa umma waliokuwa katika mafunzo hayo kuhusu namna wanavyoweza kutekeleza majukumu yao.
Waziri wa nchi ofisi ya rais Utumishi Celina Kombani akiwa katika mafunzo hayo aliyofungua leo Jijini Dar es salaam nchini Tanzania.

Waziri wa nchi ofisi ya rais utumishi wa umma, Celina Kombani, akizungumza na waandishi wa habari (Hawapo pichani) jijini Dar es Salaam leo wakati wa mafunzo ya siku mbili kwa maofisa waandamizi wa umma, kuhusu namna wanavyoweza kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia malengo hayo.
Katika maelezo yake, waziri Kombani amewataka watumishi wa umma kuacha vitendo vya rushwa kwani serikali haitosita kuwachukulia hatua za kinidhamu na kisheria kwani vitendo hivyo vimekuwa vikikwamisha juhudi za serikali za kutoa huduma bora kwa wananchi wake.

No comments:

Post a Comment