HOME

Apr 29, 2013

SARAFU MOJA CHANGAMOTO EAC!!

Viongozi wa nchi tano za Jumuiya ya Afrika Mashariki wamemaliza mkutano wao mkuu wa 11 nje kidogo ya  jiji la Arusha nchini Tanzania bila ya kufikia uamuzi juu ya kutekelezwa kwa makubaliano ya soko la pamoja na kuanzishwa kwa sarafu ya pamoja katika nchi za Jumuiya hiyo.

Viongozi hao wamerudisha ripoti na kuwataka mawaziri wao kutatua masuala kadhaa yaliyobaki ambapo Hata hivyo viongozi hao kutoka nchi za Tanzania, Kenya, Uganda Burundi na Rwanda wamesisitiza juu ya umuhimu wa kuimarisha mazingira ya biashara huru na uwekezaji katika Jjumuia yao.

Katika mkutano huo, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya alipata nafasi ya kutoa hotuba yake ya kwanza tangu achaguliwe kuwa rais mpya wa Kenya ambapo kati ya  mengi aliyozungumza ametoa wito wa kuharakisha kutataua vikwazo vinavyodhoofisha mchakato mzima wa kuunda Jumuiya ya Afrika Mashariki.

No comments:

Post a Comment