HOME

Apr 25, 2013

WANAUME WAGUMU KUPIMA UKIMWI!!

Tume ya kudhibiti Ukimwi nchini Tanzania TACAIDS, imetoa tathmini ya mwitikio wa udhibiti wa Ukimwi, tathmini inayoonyesha kuwa idadi kubwa ya wanaume hawana tabia ya kwenda kupima mara kwa mara ili kubaini kama wamembukizwa au hawajaambukizwa virusi vya ugonjwa huo.

Mwenyekiti mtendaji wa tume hiyo Dk Fatma Mrisho ametaka kuwepo kwa mbinu za kuwashawishi wanaume kujenga tabia ya kupima na kufahamu afya zao ikiwemo afya ya uzazi.

Akizungumza jijini Dar es salaam leo, Dk Mrisho amebainisha kuwa utafiti alioufanya kwa takribani miaka 10 unaonyesha kuwa asilimia 67 ya wanouguza waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi ni wanawake.

No comments:

Post a Comment