HOME

Apr 17, 2013

MAZISHI YA MARGARET THATCHER LONDON!!

Malkia Elizabeth wa Uingereza leo alikuwa miongoni mwa watu mashuhuri waliohudhuria ibaada ya mazishi ya aliyewahi kuwa waziri mkuu wa Uingereza Margaret Thatcher ibada iliyofanyika Kanisa kuu la mtakatifu Paul jijini London.

 Wawakilishi 2300 kutoka mataifa 170 duniani waliwakilisha nchi zao katika mazishi hayo kwa aliye kuwa waziri mkuu wa Uingereza aliyekaa madarakani kwa kipindi kirefu na kufariki April 8. 

Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron amewaambia kusanyiko lililokusanyika katika kanisa hilo kuwa mazishi wa kiongozi huyo yameendana na jinsi ambavyo alijijengea heshima duniani kote.
Malkia wa Uingereza alikuwepo katika mazishi hayo
Mjukuu wa Thatcher akisema machache kuhusu bibi yake mpendwa

No comments:

Post a Comment