HOME

Mar 15, 2012

WATATU WAUAWA, WAWILI WAJERUHIWA KWA KUPIGWA NONDO MKOANI MBEYA!!

Oscar Mbalamwezi (47) mkazi wa mtaa wa Chemchemi Kata ya Igawilo jijini Mbeya aliyepigwa nondo majira ya saa saba usiku wakati akitoka kuangalia mpira juzi, akiwa amelazwa katika Hospitali ya Rufaa iliyopo jijini Mbeya.

Watu watatu wamefariki dunia Mkoani Mbeya katika matukio matatu tofauti, likiwemo la mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Daudi Mtereke (26), kuuawa na wananchi wenye hasira kali baada ya kuiba baiskeli kilabuni.


Tukio hilo limetokea majira ya saa 5:30 usiku huko katika Kijiji cha Nyeregete wilaya ya Mbarali mkoani hapa, ambapo marehemu alifikwa na mauti hayo baada ya kupigwa na wananchi hao, kwa kosa la kuiba baiskeli inayomilikiwa na Bwana Siwajibu Mwihula (22) mkazi wa kijiji hicho.

No comments:

Post a Comment