HOME

Mar 1, 2012

MAREMA ATIMULIWA ANC!!

Kiongozi wa mrengo wa vijana katika chama tawala cha ANC nchini Africa Kusini, Julius Malema, sasa ametimuliwa rasmi kutoka chama cha ANC baada ya rufaa ya kupinga uamuzi wa kutimuliwa kwake hapo awali, kutupiliwa mbali.


Kamati ya nidhamu ya chama cha ANC ilitoa uamuzi huo baada ya kusikiliza rufaa iliyowasilishwa na Malema dhidi ya kutimuliwa kwake chamani kwa kipindi cha miaka mitano kwa makosa ya kuleta mgawanyiko katika ANC.


Kamati hiyo ikiongozwa na kiongozi mkongwe na mfanyibishara Cyril Ramaphosa, iliangalia tena rufaa aliyokata Bw Malema na bado ikampata na makosa ya kukigawanya chama cha ANC pamoja na kukitia aibu.
Julius Malema

No comments:

Post a Comment