HOME

Mar 28, 2012

MALI YASIMAMISHWA UANACHAMA ECOWAS!!

Jumuiya ya Afrika Magharibi ECOWAS imesimamisha uanachama wa Mali kuafuatia hatua ya jeshi kuoindua serikali ya Rais Amadou Toumani Toure .


Viongozi wa Jumuiya hiyo walifikia uamuzi huo katika mkutano uliofanyika nchini Ivory Coast.


Sasa viongozi hao kutoka nchi sita wanachama wa ECOWAS wamepanga kusafiri hadi mjini Bamako Mali ili kukutana na baraza kuu la jeshi linalotawala nchi hiyo.


Akihutubia waandishi wa habari baada ya mkutano huo Rais wa Ivory Coast, alisema Amadou Toumani Toure bado yuko hai na yuko katika hali njema .

No comments:

Post a Comment