HOME

May 30, 2012

MZEE MANDELA KUREJEA KUISHI KIJIJI ALICHOKULIA!!

Rais wa Afrika Kusini Bw. Jacob Zuma amesema Mzee Nelson Mandela atahamia katika makazi yake ya tangu utotoni katika kijiji cha Qunu na kuongeza kuwa mwasisi huyo wa taifa yupo katika afya njema.

Mandela amekuwa akiishi nyumbani kwake jijini  Johannesburg wakati makazi ya kijiji cha  Qunu, yaliyopo Mashariki mwa jimbo la Capetown yamekuwa yakifanyiwa ukarabati.

Msemaji wa rais Bw. Mac Maharaj amekaririwa na shirika la habari la
SAPA akisema kuwa mzee Mandela ameonyesha nia yake ya kutaka kurejea kijiji cha Qunu ambacho amekulia.

No comments:

Post a Comment