HOME

May 22, 2012

BOMOA BOMOA YAWAKUMBA WASUSI AMANA!!

Askari wa jiji wakiwa kazini kubomo vibanda vya wasusu maeneo ya Ilala Amana leo asubuhi
Wajasiriamali wanaojishughulisha na biashara ya ususi pembezoni mwa ukuta wa amana Ilala jijini Dar esa salaam nchini Tanzania mapema leo asubuhi wamekumbwa na dhahama ya bomoa bomoa ya vibanda vya kufanyia shughuli zao kwa kile kilichoelezwa kuwa chanzo ni migogoro ya wao kwa wao.

Zoezi hilo lililofanyika mapema leo limeelezwa kuwa chanzo chake ni kutoelewana wao kwa wao ambapo Manispaa ya Ilala imeamua kuchukua uamuzi wa kutatua mgogoro huo kwa kubomoa vibanda kitendo kilichoelezwa na wasusi ni kuepusha athari nyingine kubwa ambayo ingeweza kutokea kutokana na ubabe wa wachache kuwanyanyasa wasio kuwa na uwezo.

No comments:

Post a Comment