HOME

May 22, 2012

RAIS WA MUDA MALI ASHAMBULIWA NA WAANDAMANAJI!!

Rais wa muda Mali Bw. Dioncounda Traore
Wakuu wa serikali nchini Mali wamesema kuwa Rais wa muda wa nchi hiyo Bw. Dioncounda Traore amepelekwa hospitali akiwa na jeraha kichwani baada ya kushambuliwa na mamia ya waandamanaji.

Rais huyo anadaiwa kuwa alikuwa amezirai wakati anafikishwa hospitalini hapo lakini baadae aliruhusiwa.

Jeshi la nchi hiyo limesema kuwa limewauwa kwa kuwapiga risasi watu watatu wakati wa maandamano hayo makubwa yaliyosababishwa na kupinga mkataba ulioafikiwa kwa Bw. Traoure kuendelea kutawala kwa hadi mwaka mmoja badala ya siku 40 pekee zilizokubaliwa miezi miwili iliyopita.

No comments:

Post a Comment