HOME

May 7, 2012

MESSI AVUNJA REKODI YA DUNIA!!

Mshambuliaji Lionel Messi alifunga mabao manne na kutegeneza rekodi mpya yakufunga mabao 72 msimu huu na kumwanga kocha wa Barcelona, Pep Guardiola kwa ushindi 4-0 dhidi ya Espanyol ukiwa ni mchezo wao wa mwisho kucheza Camp Nou msimu huu.

Messi alifunga mabao hayo na kutoa zawadi kwa kocha wake aliyemsaidia Margentina huyo kuwa mchezaji bora wa dunia na Barcelona kuwa timu bora zaidi duniani.

Baada ya kufunga bao lake la 50 katika La Liga msimu huu, Messi alikimbia na kumrukia Guardiola, ambaye anaondoka baada ya kutwaa mataji 13 katika misimu nne.

Mchezaji mwingine aliyefunga mabao 70 katika msimu moja wa ligi daraja la kwanza ni Archie Stark akiwa na timu ya Bethlehem Steel iliyokuwa ikishiriki Amerikani Soka Ligi (MSL) ulikuwa ni msimu wa 1924-25.

No comments:

Post a Comment