HOME

May 22, 2012

DALADALA YAZAMA MTARONI JIJINI DAR!!

Picha juu na chini wananchi waliofika eneo la tukio wakijaribu kulitoa gari hilo wakisaidina Break down
Daladala moja linalofanya safari zake kati ya Ubungo-Msasani jijini Dar es salaam lenye namba za usajili T774 BKE lililokuwa likijaribu kulipita jingine limepinduka na kuingia mtaroni katika eneo la Makutano ya barabara ya ubalozi wa Marekani na Old Bagamoyo.

Ajali hiyo imetokana na kile kilichodaiwa kitendo cha maderez=va wanaoendesha daladala kushindana kuwahi abiria kutoka kituo kimoja hadi kingine na kuendelea kusababisha ajali mbalimbali kutokana na haraka na kupita barabara zisizo sahihi.

Abiria waliokuwa ndani ya gari hilo wameumia na kupata majeraha madogo madogo ambapo mashuhuda wamesema uzembe wa dereza wa gari hilo umesababisha ajali hiyo.

No comments:

Post a Comment