HOME

May 9, 2012

RAIS KIKWETE AWASILI ADDIS ABABA KWA KONGAMANO LA UCHUMI LA KIMATAIFA KWA AFRICA!!


 "Karibu Mheshimiwa...." Anaonekana kusema Mkurugenzi wa World Economic
Forum kwa Afrika Bi Elsie Kanza wakati wa kumpokea Rais Jakaya Kikwete
alipowasili hoteli ya Sheraton jijini Addis Ababa usiku wa kuamkia leo
April 9, 2012 tayari kuhudhuria Kongamano la Uchumi la Kimataifa kwa Afrika
linaloshirikisha zaidi ya viongozi 700 wa nchi, biashara na uchumi kutoka
sehemu mbalimbali duniani.
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa USAID Dkt Rajiv
Shah katika hoteli ya Sheraton jijini Addis Ababa leo April 9, 2012 ambako
kwa pamoja wanahudhuria Kongamano la Uchumi la Kimataifa kwa Afrika
linaloshirikisha zaidi ya viongozi 700 wa nchi, biashara na uchumi kutoka
sehemu mbalimbali duniani
Rais Jakaya Kikwete katika maungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa USAID Dkt
Rajiv Shah katika hoteli ya Sheraton jijini Addis Ababa leo April 9, 2012
ambako kwa pamoja wanahudhuria Kongamano la Uchumi la Kimataifa kwa Afrika
linaloshirikisha zaidi ya viongozi 700 wa nchi, biashara na uchumi kutoka
sehemu mbalimbali duniani.(PICHA NA IKULU)

No comments:

Post a Comment