HOME

May 24, 2012

RAIA WA MISRI WAENDELEA KUPIGA KURA!!

Zoezi la upigaji kura katika siku ya kwanza lilikwenda vizuri kwa utulivu katika maeneo mengi lakini waandamaji walirusha viatu na mawe katika ujumbe wa mgombea Ahmed Shafiq ambaye alikuwa waziri mkuu wa mwisho katika utawala wa Mubarak.

Baraza la kijeshi lililochukua madaraka mwezi Februari mwaka 2011 limeaahidi uchaguzi wa haki na utawala wa kiraia ambapo zoezi la upigaji kura lilianza jana kwa misururu mirefu iliyoonekana katika baadhi ya vituo vya kupigia kura.

Misururu mirefu imeonekana katika baadhi ya vituo vya kupigia kura na vyombo vya habari vimeripoti kuwa idadi kubwa ya watu wamejitokeza kuliko jana.

No comments:

Post a Comment