HOME

May 24, 2012

MNYIKA ASHINDA KESI!!

Mamia ya wafuasi wa CHADEMA wakiwa wamembemba mbunge John Mnyika ambaye ameshinda kesi katika hukumu iliyotolewa katika mahakama kuu kanda ya Dar es salaam.
Mbunge wa jimbo la ubungo nchini Tanzania John Mnyika, ameshinda shauri la kupinga ubunge wake liliofunguliwa katika mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam na aliyekuwa mgombe kupitia Chama Cha Mapinduzi Bi. Hawa Ng'umbi.

Jaji wa mahakama kuu, Upendo Msuya ametupilia mbali hoja zote tano zilizofikishwa mahakamani hapo na upande wa mashtaka kwa madai kuwa hoja hizo hazina msingi.

Akizungumza. Muda mfupi baada ya kutolewa kwa hukumu hiyo, mwenyekiti wa Chadema taifa, Freeman Mbowe amesema ushindi wa kesi hiyo ni ushindi kwa Watanzania wote huku akionyesha kusikitishwa na jinsi nchi inavyoingia hasara kwa kutumia kiasi kikubwa cha pesa kuendesha kesi zisizo na msingi.

No comments:

Post a Comment