HOME

May 10, 2012

MWENGE WA OLIMPIKI WAWASHWA UGIRIKI!!

Moto wa mwenge utakaotumiwa kuwasha mwenge wa mashindano ya Olimpiki mjini London uliwashwa mahali yalipozaliwa mashindano ya kale ya Olimpiki siku ya Alhamisi.

Muigizaji mwanamke, aliyevalia kama mtawa mwanamke wa enzi za miungu wa Kigiriki alitumia kioo kupokea mwanga wa jua na kuasha mwenye.

Kukiwa na jua la kutosha angani, hapakua na sababu ya kutegemea moto kutoka kwingine wakati wa kufanya majaribio ya mwisho kuasha mwenge wa Olimpiki siku moja kabla.

Baada ya sherehe za kufana, mtawa huyo atakabidhi mwenge kwa mtu wa kwanza kutembeza mwenge huo, mwanariadha muogeleaji kutoka Ugiriki aliyeshinda medali ya fedha kwenye mashindano yya Olimpiki Spyros Gianniotis.

No comments:

Post a Comment