HOME

May 24, 2012

TWIGA STARS YAKABIDHIWA BENDERA!!

Timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya wanawake (Twiga Stars)  imekabidhiwa Bendera ya Taifa  tayari kuelekea nchini Ethiopia kucheza na timu ya nchi hiyo  katika mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya mchujo wa kucheza  Fainali za Nane za Kombe la Afrika kwa Wanawake (AWC) zitakazofanyika Novemba mwaka huu Equatorial Guinea.

Akikabidi bendera hiyo  Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mhe. Amos Makalla amesema anaamini wachezaji wamepata uzoefu wea kutosha katika michezo ya majaribio waliyocheza licha ya kufungwa..

Kwa upande wake kocha wa Twiga stars ameonyesha matumaini makubwa ya kushinda mchezo huo licha ya kuanzia ugenini.

Mechi hiyo itafanyika Mei 27 mwaka huu kwenye Uwanja wa Addis Ababa wakati ile ya marudiano itachezwa Juni 16 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Twiga Stars ikifanikiwa kuitoa Ethiopia itakuwa imepeta tiketi ya kwenda Equatorial Guinea.

No comments:

Post a Comment