HOME

May 21, 2012

WILL SMITH AMNASA KIBAO MWANDISHI WA HABARI!!

Mwanamuziki na mcheza filamu kutoka nchini Marekani Will Smith ameripotiwa kwa tukio la kumnasa kibao mwandishi wa habari raia wa Ukraine, Vatalii Sediuk, baada ya jaribio lake la kumbusu mdomoni nyota huyo kushindikana.

Smith kwa sasa yupo katika kampeni na vyombo vya habari kutangaza toleo lake la tatu la filamu ya Men In Black ambayo inatarajiwa kutoka rasmi mei 25.

Katika Red Carpet party iliyofanyika huko Moscow, Seiduk wakati akikumbatiana na Will Smith alijaribu kumbusu Smith mdomoni, kitendo ambacho kilimuudhi na kumshangaza sana hadi kushindwa kujizuia kurusha kofi.

No comments:

Post a Comment