HOME

May 5, 2012

GEREZA LASHAMBULIWA NIGERIA!!

Watu waliokuwa na silaha wamevamia gereza nchini Nigeria katika jimbo la Borno, kaskazini-mashariki mwa nchi, na kuwauwa walinzi wawili, na kuwaachilia huru wafungwa.

Polisi walisema wapiganaji wa kikundi cha Waislamu cha Boko Haram walishambulia kituo cha polisi kwenye mji wa Banki, kabla ya kuelekea gerezani karibu na kijiji cha Kunshi.

Hakuna aliyedai kuhusika na shambulio hilo, lakini Boko Haram imelaumiwa kwa matukio kadha ya mauaji nchini Nigeria.

No comments:

Post a Comment