HOME

May 24, 2012

QATAR, DOHA, BAKU NA AZERBAIJAN NJE KATIKA KINYANG’ANYIRO CHA KUANDAA OLIMPIKI 2020!!

Miji ya Tokyo, Madrid na Istanbul ndiyo iliyobakia katika kinyang’anyiro cha kuwania nafasi ya kuandaa mashindano ya Olimpiki ya mwaka wa 2020.

Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki – IOC iliyokutana mjini Quebec nchini Canada imepunguza orodha ya miji iliyokuwa ikiwania nafasi hiyo, ambapo mji mkuu wa Qatar -Doha, Baku na Azerbaijan imeondolewa katika orodha hiyo.

Kamati ya Olimpiki itafanya maamuzi ya mwisho mnamo Septemba 7 mwaka 2013, kuhusu mji upi upewe fursa ya kuandaa mashindano ya Olimpiki ya majira ya joto yatakayofanyika mwaka 2020. 

Mashindano ya mwaka huu yatafanyika katika jiji London nchini Uingereza.

No comments:

Post a Comment