HOME

May 7, 2012

WAZIRI MKUU ODINGA AIFUKUZA BODI YA NHIF KENYA AKIKINZANA NA KAIMU MKUU WA UTUMISHI WA UMMA ALIYEIREJESHA KAZINI!!

Waziri mkuu wa Kenya Raila Odinga leo ameifukuza kazi bodi ya mfuko wa taifa wa bima ya afya na mtendaji wake mkuu kufuatia uamuzi wa waziri wa huduma za jamii Anyang' Nyong'o.

Waziri mkuu Odinga amemteua kaimu katibu mkuu wa wizara hiyo A. Adan kuwa kaimu mkurugenzi mkuu ambapo pia ameiteua bodi ya uangalizi inayoundwa na makatibu wakuu na wawakilishi kutoka vyama vya Cotu na Knut.

Tangazo la waziri mkuu Odinga linakinzana na tangazo la kaimu mkuu wa utumishi wa umma Francis Kimemia la kuifukuza bodi hiyo na mkurugenzi wake mkuu.        

No comments:

Post a Comment