HOME

May 21, 2012

MWASISI WA FACEBOOK AFUNGA NDOA NA MPENZI WAKE WA SIKU NYINGI!!

Mwasisi wa mtandao maarufu wa kijamii Facebook Mark Zuckerberg amefunga ndoa mwishoni mwa wiki iliyopita na mpenzi wake wa siku nyingi Priscilla Chan, Harusi hii imeripotiwa kuwa ya kipekee na mvuto mkubwa katika mitandao mbalimbali ya burudani ya kimataifa.

Wawili hawa walikutana huko Harvard na wamekuwa pamoja kwa miaka 9 sasa, kabla ya kuamua kufunga ndoa na kufanya sherehe ndogo nyumbani kwa Zuckerberg huko Palo Alto, Calif.

Mke wa Zuckerberg alihitimu masomo yake ya udaktari katika chuo cha California muda mfupi kabla ya harusi yake na majirani waliyoizugumzia sherehe ya harusi hiyo wamesema kuwa walisikia miziki mbalimbali ya wasanii kama Flo Rida, Bon Jovi na Janet Jackson ila miziki iliyopigwa zaidi ilikuwa ni ile ya marehemu Michael Jackson.

No comments:

Post a Comment