HOME

May 27, 2013

SHUHUDIA WILL SMITH AKIPIGA PENALTY KWENYE SHEREHE ZA FAINALI YA UEFA CHAMPIONS LEAGUE.

Kuelekea fainali ya UEFA Champions League iliyopigwa juzi na Bayern Munich kuukwaa uchampion wa Ulaya, staa wa Hollywood Will Smith na mwanae Jaden Smith walipata nafasi ya kushiriki the Ultimate Champions Match ambayo pia ilishirikisha wakali wa zamani kama Luis Figo, Gianfranco Zola na Robert Pires.


Isivyotegemewa na wengi, baba na mwana Smith walijikuta wakiiba show nzima kutokana na vimbwanga vyao katika uchezaji mpira hasa penalty.

Kati ya penalty KUMI walizopiga, walifanikiwa kumfunga goli moja tu, Edwin Van De Sar aliyekuwepo golini, baada ya Will Smith kuamua kumzuia asidake penalty hiyo.

Fuatilia video ya tukio hilo kwa ufupi hapa chini.

No comments:

Post a Comment