HOME

May 28, 2013

PICHA: OMBAOMBA ASHUSHIWA KICHAPO BAADA YA KUJIFANYA MLEMAVU!





















Mzee Mmoja ambaye amekuwa akiigiza ni mlemavu asiye na mguu mmoja na mkono mmoja ameambulia kichapo cha wananchi wenye hasira kali wa kijiji cha Miyomboni mjini Iringa.

Tapeli  huyo  mbali ya kuumbuliwa kwa kutakiwa kuonyesha miguu  yake yote pamoja na mikono yake yote bado amepata kuchezea  kichapo kiasi cha kunusurika kuuwawa na wananchi hao wenye hasira kali.

Tukio la mzee huyo kubainika kama ni tapeli kwa mara ya kwanza  mtandao wa www.francisgodwin.blogspot.com na www.matukiodaima.com ndio ulipata kufichua siri hiyo ya omba omba huyo kuwa si omba omba kutokana na kumnasa akijiweka mfano wa mlemavu .

Kutokana na kufichuliwa kwa siri hiyo ya kujiigiza kuwa ni omba omba mlemavu wananchi wamekuwa wakimtimua kila kona anayokaa tapeli huyo na kumtimua mbio kabla ya leo wananchi hao kuamua kumkimbiza kutoka eneo la Hazina Ndogo hadi Miyomboni na kuanza kumpa kichapo hadi alipoamua kuonyesha viungo vyote kuwa si mlemavu.

Tapeli huyo mbali ya kujifanya ni mlemavu wa viungo wakati mwingine huwa anajifanya ni mtu asiyeongea (bubu) asiye na viungo kama mikono na miguu ila wakati mwingine akijifanya ni hana mguu mmoja na kuwaomba watu fedha za matibabu .




Kwa hisani ya http://iringa-yetu.blogspot.com

No comments:

Post a Comment