HOME

Jun 20, 2012

SUPER NYAMWELA AOA KINYEMELA!!

Super Nyamwela
Mnenguaji na mwanamuziki mahiri wa bendi ya muziki wa dansi nchini Tanzania ya Extra Bongo Next Level Wazee wa Kizigo, Super Nyamwela hatimae amevuta jiko lake la pili na safari hii ameamua kufanya siri.

Ndoa hiyo imefungwa kwa siri ambapo baadhi ya watu wameshangaa kutoalikwa kwenye sherehe ya ndoa hiyo iliyofungwa juzi Jijini DSM.

Hivi karibuni mnenguaji huyo aliwahi kufunguka kwenye kipindi cha Mkasi kinachorushwa na East Africa Tv kuwa baada ya aliyekuwa mke wake kufariki miaka kadhaa iliyopita anatarajia kufunga pingu za maisha na mpenzi wake ili waweze kumlea mtoto wake.

No comments:

Post a Comment