HOME

Jun 25, 2012

WATU WATATU WAMEKUFA KATIKA SHAMBULIO LA BOMU MOMBASA!!

Watu wengine wawili wamekufa na kufanya idadi ya waliokufa katika shambulio la bomu lililotokea Mombasa nchini Kenya siku ya Jumapili kufikia watatu huku wengine 25 wakipatiwa matibabu katika hospitali ya Jimbo la Pwani baada ya kujeruhiwa.


Tukio hilo ambalo limetokea saa nne kamili usiku limetokea katika baa moja wakati watu wakiangalia mechi ya mpira wa miguu.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema waliona wanaume wawili na mwanamke mmoja wakiwasili ndani ya gari aina ya Rav 4 na kushuka kuelekea baa hiyo na baadae mlipuko huo ulitokea na gari kutokomea.

Mlipuko huo umetokea saa chache baada ya serikali ya Marekani kutoa tahadhari ya ugaidi na kuonya raia wake kuwa waangalifu katika Pwani ya Kenya.

No comments:

Post a Comment