HOME

Jun 20, 2012

TANZANIA KUTORIDHIA MISAADA YA MASHARTI KUHALALISHA USHOGA!!

Waziri wa Mambo ya Nje Mhe. Bernad Membe
Serikali ya Tanzania imesema iko tayari  kujifunga mikanda na kujibeba yenyewe kuhakisha haikubali kudhalilishwa kiutu na utamaduni wake kwa kukubali kupokea misaada ya masharti itakayotulazimisha kukubaliana na  ndoa za jinsia moja. 

Kauli hiyo imetolewa bungeni mjini Dodoma na Waziri wa Mambo ya Nje Mhe. Bernad Membe wakati akijibu swali la mbunge wa Konde Mh. Khatib Said Haji aliyetaka kujua serikali imejipanga vipi kukabiliana na   janga la nchi wahisani watakapotoa misaada  yao kwa lengo la kushinikiza ndoa  za jinsia moja.

Akijibu swali hilo Mh. Membe amesema dini zote  hapa nchini hazikubaliani  na uwepo wa ndoa ya jinsia  moja  na viongozi wake wapo mstari wa mbele kukemea  jambo hili na kwa maana hiyo utamaduni wa  nchi  na  sheria za dini hazitambui ndoa ya jinsia moja.

No comments:

Post a Comment